Kusimamia utekelezaji wa Sera ya Elimu katika mfumo rasmi na
Elimu nje ya mfumo rasmi katika manispaa. Aidha ni pamoja na
kuandaa.
1. Kuandikisha watoto wa darasa la kwanza wenye umri wa miaka
wa kwenda shule.
2. Kuelimisha jamii kushiriki katika mambo mbali mbali ya shule
kupitia vikao vya mitaa ambavyo wananchi watahudhuria na
kutoa maoni.
3. Kuandaa bajeti ya idara na vitengo vyake ikiwa ni pamoja na
mpango kazi unaoendana na bajeti hiyo.
4. Kusimamia na kuendeleza taaluma katika manispaa ya musoma
kwa kusimamia ufundishaji, ujifunzaji mahudhurio ya walimu,
wanafunzi na utendaji kazi kwa ujumla.
5. Kuandaa takwimu mbalimbali za kielimu za wanafunzi, walimu,
samani na miundombinu.
6. Kuratibu mashindano ya ya taaluma na michezo kwa shule za
msingi.
7. Kusimamia haki na maslahi ya walimu kwa kufuata taratibu
kama vile ruhusa, likizo masomo, matibabu n.k.
8. Kuhudumia jamii kuhusiana na mambo yote ya kielimu na
mafunzo mbalimbali kupitia kamati za shule na shuguli
nyinginezo kama vile uhamisho wa wanafunzi.
9. Kuandaa na kuendesha vikao mbalimbali vya wadau wa elimu
katika ngazi zote za manispaa.
10. Kuandaa Tange ya walimu wa shule za msingi kwa kila mwaka.
Barabara ya Kuelekea Kanisa la Katoliki Kipingo
Postal Address: P.O.BOX 18 Malinyi
Telephone: 255
Mobile: 0755388218
Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz
Hatimiliki©2017 MALINYIDC Haki zote zimehifadhiwa