Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mheshimiwa Sebastian Waryuba amezindua rasmi zoezi la umezaji Dawa za Minyoo ya Tumbo na Kichocho tarehe 12 Februari 2026 katika Shule ya Msingi Ngongwa.
Zoezi hili linatarajiwa kuwafikia jumla ya Wanafunzi 40,193 wenye umri wa miaka 5 hadi 14 katika shule zote za Msingi Wilayani Malinyi. Katika Kampeni hii Wanafunzi wanapatiwa dawa za Albendazole kwa ajili ya minyoo ya tumbo na Praziquantel kwa ajili ya Kichocho, kwa kuzingatia miongozo ya Wizara ya Afya. Lengo la zoezi hili ni kudhibiti na kupunguza maambukizi ya magonjwa haya, kulinda afya za watoto wetu, kuboresha ukuaji wao na kuongeza uwezo wa kujifunza shuleni.
Ushirikiano wa Serikali, Walimu, Wahudumu wa Afya, Wazazi ni nguzo muhimu katiks kuhakikishs mafanikio ya kampeni hii.
Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi
Postal Address: 18 Malinyi, Morogoro
Telephone: 0643111999
Mobile:
Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz
Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.