Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Ndugu Khamis Katimba amefungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba na Darasa la Nne kwa mwaka 2024 na 2025. Kikao hiko kimefanyika katika Ukumbi wa Ngakawa Malinyi tarehe 9 Februari 2025.
Katika hotuba yake ya Ufunguzi DED Khamis Katimba amesema moja ya ndoto yake ni kuifanya Halmashauri ya Malinyi kupaa kimichezo.
DED Khamis Katimba pia aliwausia Washiriki wawe na nidhamu kwenye kila kitu kuanzia kwenye uandaaji wa masomo, ufundishaji, mahusiano nk.
Aidha DED Katimba amewataka Wakuu wa Shule washuke chini kwa Walimu wao, wajishushe ili wajue wana matatizo gani ili waweze kujua changamoto zao na kuzishughulikia amesisitiza hakuna kinachoharibika kwenye kujishusha na pia ametaka kila mtu am bane mwenzake kwenye kutimiza wajibu wake.
Kuhusu Usimamizi wa Miradi DED Katimba amesema Serikali inaleta Fedha za kujenga Miradi inatakiwa isimamiwe vizuri "Performance depend on Academic and non Academic factor" hivyo ukishakuwa Mwalimu Mkuu wewe tayari ni Engineer, Accountant, Procurement nk. Ukizembea unaiweka nafasi yako kwenye Mtihani hivyo ni lazima Walimu Wakuu wajiongeze wasifikirie KKK tu.
Kwa upande wa Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi Ndugu Maajabu Nkanyemka amesema Kikao hiko kitatoa Dira namna wanavyoupokea mwaka mpya na ni faraja kwa Ufaulu wa asilimia 95.73% Darasa la Saba na Asilimia 94.04% Darasa la Nne mwaka 2025. Amemuomba Mwenyezi Mungu awape ujasiri na nguvu ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa mwaka 2026.
Kikao Kazi hiko kimejadili na kufanya tathmini ya Matokeo ya Darasa la Saba na la Nne 2025 na Mikakati ya 2026, Mrejesho wa Kikao cha Utekelezaji Robo ya 2 ( Gairo) na Mrejesho wa Kikao cha Maafisa Elimu Taaluma cha tarehe 2/02/2026, Miradi ya Maendeleo, Michezo, Mitihani ya Utamirifu (Kalenda) 2026, Lishe na Utoaji taarifa za Robo Wiki. Pia Washiriki walipata wasaa wa kupata maelekezo kutoka Ofisi za Utumishi, Udhibiti Ubora wa Shule na TSC.
Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi
Postal Address: 18 Malinyi, Morogoro
Telephone: 0643111999
Mobile:
Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz
Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.