Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mheshimiwa Sebastian Waryuba ameongoza Kikao cha Ushauri cha Wilaya kujadili Rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.
Katika Kikao hiko Washiriki walipata nafasu ya kujadili kwa kins utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 Kipindi cha Nusu Mwaka ( Julai 1,2025 hadi Disemba 31,2025 na mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2026/2027.
DC Waryuba ametoa maelekezo kama ifuatavyo katika Kikao hiko
Ametaka vibali vya sherehe visimamiwe na Sherehe ziwe na maadili watoto wadogo wazuiwe kushiriki.
Ameitaka Halmashauri iunde Mfuko wa Elimu" Malinyi Education Development Fund" amesema utapunguza changamoto za Walimu na Lishe Mashuleni.
Amewataka Wataalamu waandae takwimu sahihi mfano za Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Amewataka Watendaji Kata wote wapate takwimu za Watoto wote walioripoti shule mpaka wiki ya Pili Februari, Wazazi wa watoto wasioripoti wakamatwe.
Amewaomba Wananchi wajiandikishe kwenye Bima ya Afya ya Wote (NHIF) na pia wajiandikishe kwenye Daftari la Wakazi.
Amesisitiza kusimamia Lishe kwa Watoto Mashuleni na Wazazi ni lazima wapeleke chakula mashuleni.
Watendaji Kata kufikia tarehe 15 Februari 2026 walete orodha ya Guest zote zilizopo ndani ya Halmashauri ya Malinyi.
Mkaguzi wa Ndani "Internal Auditor" awe anaenda kukagua Watendaji wa Vijiji kabla ya kuhama vituo vya kazi.
Upangaji wa Minada ya Mifugo unatakiwa ufuate soko linavyokwenda.
Watendaji wa Kata na Vijiji wahamasishe Wananchi wajiandikishe kwenye mfumo wa Wazabuni (Nest)
Watoa Huduma ndani ya Halmashauri ni lazima walipe "Service Levy" kwa mujibu wa sheria.
Halmashauri itengeneze Rasimu ya Bajeti iboreshwe kwani itapimwa kwa namna ilivyokusanya mapato na ilivyotumia.
Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi
Postal Address: 18 Malinyi, Morogoro
Telephone: 0643111999
Mobile:
Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz
Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.