madiwani wa halmashauri ya wilaya ya malinyi wamejifunza mfumo wa stakabadhi ghalani kwa lengo wilayani Tandahimba kwa lengo la kuboresha mfumo wa makusanyo ya fedha katika mazao yanayolimwa wilayani Malinyi,Tandahimba ni wilaya ambayo imefanikiwa katika ukusanyaji wa fedha za mazao kama korosho na ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.
Mafunzo hayo ni mahususi kwa ajili ya kufanikisha mfumo wa stakabadhi ghalani ambao katika msimu wa kilimo uliopita wa mwaka 2021/2022 ulitumika kuuzia zao la koroshokatika chama kikuu cha ushirika cha Ulanga kilombero ambacho ni chama kikuu cha wilaya tatu za Malinyi, kilombero na Ulanga.
akizungumza katika mafunzo hayo, mwenyekiti wa Halmashauri ya Tandahimba mh.Baisa Baisa amesema mfumo wa huo wa stakabadhi ghalani ghalani ukisimamiwa vema unaweza kusaidia upatikanaji wa mapato makubwa.kutokana na hoja hizo zilizotolewa na mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi walitaka kujua namna ya kukusanya Kodi mbalimbali za zao la korosho ambalo ndilo hasa lililoingizwa katika mfumo huu wilayani Malinyi.ambapo Mwanasheria wa Halimashauri hiyo ya Tandahimba akijibu hoja za madiwani hao amewataka madiwani wa malinyi kuhamasisha wananchi kulima mazao ambayo wanalenga kuyauza katika mfumo wa stakabadhi ghalani. ambayo ni ufuta na korosho lakini pia ameshauri Halmashauri ya wilaya ya Malinyi kutengeneza mfumo maalumu wa uuzaji wa zao la mpunga ambalo ndilo zao kuu la kilimo wilayani malinyi.
Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi
Postal Address: 18 Malinyi, Morogoro
Telephone: 0643111999
Mobile:
Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz
Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.