• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Malinyi District Council
Malinyi District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Mipango
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Machine Investment
    • Skimu ya Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili Madiwani
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Kata
      • Biro
      • Igawa
      • Itete
      • Kilosa Mpepo
      • Mtimbira
      • Malinyi
      • Njiwa
      • Ngoheranga
      • Sofi
      • Usangule
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Matamko ya mbalimbali
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video

Malinyi Yaadhimisha Wiki ya Sheria

Posted on: February 1st, 2023

Viongozi na wadau mbalimbali wilayani malinyi mkoani morogoro wametakiwa kuongeza juhudi katika kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi badala ya kuitumia mahakama kama njia pekee ya kupata haki.

Akizungumza katika maadhimisho ya wiki ya siku ya sheria nchini yaliyofanyika kiwilaya katika viwanja vya mahakama vilivyopo katika kijiji cha nawigo wilayani hapa, mwakilishi wa mkuu wa wilaya Bi Rehema Rajabu amesema uendeshaji wa kesi mahakamani hutumia muda mrefu pamoja na rasilimali fedha hivyo kuchangia kudumaa kwa maendeleo ya watu.

Bi Rajabu amesema ili kuwe na uchumi imara wa mtu mmoja mmoja, wilaya mkoa na taifa kwa ujumla ni muhimu kuwe na utatuzi wa migogoro kwa njia usuluhishi ambayo ni rahisi, haina gharama na inaokoa muda hali itayopelekea kurejea kwa amani miongoni mwa wanajamii na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi.

Aidha Bi Rajabu ameitaja migogoro ya umiliki wa ardhi, mirathi pamoja na migogoro ya wanandoa kuwa ndio migogoro mikubwa inayojitokeza mara nyingi katika maeneo mengi wilaya hapa na hivyo kutoa rai kwa wananchi kutafakari kwa kina suala utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhisi kabla ya kufikiria kwenda mahakamani.

Kwa upande wake hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya Bwana Samweli Obasi amesema utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi ni takwa la kikatiba ambalo utekelezaji wake ni muhimu kwa kasi ya ukuaji wa shughuli za kiuchumi hapa nchini.

Katika hatua nyingine Bwana Obasi amesema utatuzi wa migogoro nje ya mahakama imekuwa ni namna mbadala ya chombo kikuu cha kuifikia haki kwa wakati na kuendeleza kasi ya maendeleo ya kiuchumi kwa kutoa wasaa kwa watu kutekeleza shughuli zao za kujiongezea kipato jambo ambalo huipa serikali mapato na uchumi wa nchi kukua.

Kuadhimishwa kwa wiki ya sheria kunafungua mwaka mpya wa kazi za mahakama kote nchini.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2020/2021 December 18, 2020
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2020 January 17, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI January 18, 2021
  • Tangazo la Nafasi za kazi May 26, 2022
  • Angalia yote

Habari za hivi punde

  • Kitengo cha macho hospitali ya wilaya ya malinyi chazinduliwa na kufanya upasuaji wa kwanza

    March 20, 2023
  • Kitengo cha macho hospitali ya wilaya ya malinyi chazinduliwa na kufanya upasuaji wa kwanza

    March 20, 2023
  • Madiwani wafanya ziara ya mafunzo Tandahimba

    March 02, 2023
  • katibu mkuu CCM Awaasa Viongozi/Wanachama Malinyi

    February 03, 2023
  • Angalia yote

Video

DAS MALINYI AKIKABIDHI PIKIPIKI KWA WARATIBU ELIMU KATA
Video zaidi

Tovuti za haraka

  • Matangazo
  • Habari za Hivi punde

Tovuti Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Tovuti ya Ajira
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2022
  • Matokeo ya Kidato cha Nne
  • SALARY SLIP PORTAL
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2018

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi

    Postal Address: 18 Malinyi, Morogoro

    Telephone: 0643111999

    Mobile:

    Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.