Katibu mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Taifa Daniel Chongolo amewataka viongozi za vijiji kutokuwa chanzo cha migogoro katika maeneo yao na badala yake wanapaswa kuwa suluhu ya udhibiti wa migogoro hiyo kwa wananchi.
Dkt Chongolo ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha itete wilayani malinyi mkoani morogoro katika ziara ya siku moja wilayani hapa iliyolenga kukagua miradi ya maendeleo, kusikiliza kero za wananchi na kutatua kero za wananchi pamoja na kuangalia uhai wa chama wilayani hapa.
Aidha Dkt Chongolo ameongeza kuwa ukiona katika kijiji kuna mgogoro ama wa wakulima na wafugaji au mgogoro wa ardhi kati ya mwananchi mmoja na mwingine basi ujue uongozi wa eneo hilo unatatizo na hivyo akawataka viongozi wa vijiji kuongoza kwa kuzingatia haki na utawala bora.
Katika hatua nyingine Dkt Chongolo amemuagiza mkuu wa wilaya Mh. Sebastian Waryuba kufuatilia taarifa za uwekaji wa alama za mpaka wa kwanza na wapili unaotenganisha kijiji hicho na hifadhi ya bonde la mto kilombero na kuja na majibu yaliyokamilika kwa wananchi.
Pamoja na hayo Dkt Chongolo akiwa wilayani hapa wananchi na wanachama wa chama cha mapinduzi kuwalea watoto katika maadili mema ili kuwa na jamii yenye watu waadilifu na wachapakazi na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.
Katika kuhakikisha nchi inakabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Dkt Chongolo ameuagiza umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi wilayani hapa kupanda miti katika hospitali ya wilaya pamoja na maeneo mengine ikiwa ni jitihada za kuimarisha utunzaji wa mazingira kwa ustawi wa wilaya mkoa na taifa kwa ujumla.
Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi
Postal Address: 18 Malinyi, Morogoro
Telephone: 0643111999
Mobile:
Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz
Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.