• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Malinyi District Council
Malinyi District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Mipango
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Machine Investment
    • Skimu ya Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili Madiwani
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Kata
      • Biro
      • Igawa
      • Itete
      • Kilosa Mpepo
      • Mtimbira
      • Malinyi
      • Njiwa
      • Ngoheranga
      • Sofi
      • Usangule
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Matamko ya mbalimbali
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video

Water

HALMASHAURI YA WILAYA YA MALINYI

IDARA YA MAJI

  • UTANGULIZI

Idara ya maji inajukumu la kuhakisha huduma ya maji safi na salama inapatikana kwa wananchi. Kazi ya usimamizi  na  utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya maji zinafanyika kutokana bajeti ya fedha za  programu ya maendeleo ya sekta ya maji (WSDP),Ruzuku ya maendeleo ya maji na fedha za wahisani mbalimbali.

  • Hali ya watumishi

Idara ya maji ina jumla ya watumishi 2 kati ya watumishi 13 ambao wangeweza kusimamia na kutekeleza kazi za maji. Huduma ya maji Kijamii

Na
Watumishi/kundi
Ngazi ya elimu
Idadi
1
Mhandisi wa maji
Degree
1
2
Fundi sanifu

1
















 





3.0 HALI YA HUDUMA YA MAJI

Miongozo na sera mbalimbali

Usimamizi na mipango yote ya utoaji wa huduma ya maji kwa wananchi inazingatia misingi muhimu ifuatayo. Sera ya Taifa ya maji 2002,Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025,Malengo ya Milenia,Ilani ya uchaguzi chama Tawala (CCM) 2015 na Miongozo mbalimbali inayotolewa na serikali kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo katika sekta ya maji..

 

 3.1 VYANZO VYA MAJI

Wilaya ya Malinyi inahudumia Wananchi maji kutoka kwenye vyanzo vya maji ambavyo hutokana na Mito, visima vifupi na visima virefu.

Hali ya mazingira ya vyanzo vya maji si ya kuridhisha japokua bado vinaendelea kutoa maji. kuna changamoto ya kupungua kwa baadhi ya vyanzo kulingana na mabadiliko ya hali ya hewa na tabia ya nchi,ukataji miti  pamoja na wingi wa mifugo inayoengezeka kila siku.

 3.2 HALI YA UPATIKANAJI WA HUDUMA YA MAJI

Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji maji ni ya wastani ambapo kati ya wananchi 125,504 na wananchi 67750 ndio wanaopata huduma ya maji  kiwango hiki ni sawa na  asilimia 53 ya wakazi wake. .Aidha kuna visima vifupi vya asili vilivyoboreshwa vipatavyo 50, visima vifupi vilivyofungwa pampu za mkono 206 na vituo 105 katika miradi ya maji ya kutege Itete na mtimbira na mradi wa maji ya kusukuma kwa pampu ya mafuta wenye vituo 2. Katika kijiji cha Lupunga. Visima.

Kwa ujumla kuna vituo vya kuchotea maji 420 ambapo vituo 271 ndivyo vinavyofanya kazi.   

4.0  UBORA WA MAJI

Katika kuhakikisha kuwa usalama wa maji unaendelea kuwepo halmashauri imegawa dawa aina ya chlorine  kwa miradi ya maji Itete na Mtimbira ili iwekwe kwa ajilia ya kutibu maji kabla hayajagawiwa kwa wananchi. Aidha visima vifupi na virefu huwekwa dawa aina hiyo kabla kuanza kutumika pindi vinapo chimbwa.

4.1 USHIRIKIANO NA WADAU WENGINE WA MAENDELEO

Halmashauri kupitia  maandiko na vikao mbalimbali  vya wadau wa  kuongeza kiwango cha utoaji na upatikanaji wa huduma ya maji. Aidha wadau wafuatao wameonyesha nia ya kusaidia  upatikanaji wa maji ambapo  (CARITAS) wamesaidia uchimbaji wa visima vifupi 6 Ihowanja 4 na Mabanda 2. Wengine ni Lions Pure Water ambao wameonyesha nia ya kusaidia mradi wa maji ya Bomba Sofi Majiji. Pamoja na Water resources integrated development initiative (WARIDI) amblo limekubali kufanya kazi na halmashauri katika maeneo ya usamamizi wa Jumuiya ya watumiaji maji nauboreshaji wa miundombinu ya maji.

 4.UTEKELEZAJI WA PROGRAMU YA MAENDELEO YA MAJI (WSDP)

Halmashauri ya wilaya ya Malinyi inatekeleza programu ya maendeleo ya sekta ya maji.

  • Mradi wa maji ya mserereko kwa vijiji vya Malinyi ,Kipingo na makerere ambao unaendelea kujengwa na ambao unasimamiwa na wilaya ya Ulanga.
  • Mradi wa uchimbaji wa visima virefu na 20 katika kata ya Mtimbira ,Usangule na katikavijiji vya Kiswago,Sofi majijiji,Sofi mission,Misegese na kilosa mpepo. Kazi hiiimeanza na inaendelea kwa mafanikio mazuri.

Pia kwa mwaka wa fedha 2016/17 ujenzi wa visima virefu 8 vilivyofungwa pampuya mkono vilijengwa katika vijiji vya Ngoheranga 5, Tanga 2 na Majiji 1.

Aidha visima vifupi 4 katiya sita vimejengwa Ihowanja 3 na Mabanda 1kwa uhisani wa Cartas. Ukarabati wa visima  8 umefanyika Misegese 1,Makerere 1,Kiswago 2,Madibira 1,Mtimbira 1,Biro 1,Mbalinyi1 na kilosa Mpepo 1. Ujenzi wa visima vifupi umefanyika Igawa sekondari na Ngombo kupitia fedha za maendeleotokaserikali kuu.

5.0 USAJILI WA VYOMBO HURU VYA WATUMIAJI MAJI (COWSOs)

Kulingana na sheria mpya ya maji ya mwaka 2009 miradi yote ya maji inabidi iundiwe vyombo huru vya watumiaji maji vitakavyopendekezwa na kukubaliwa na jamii husika kulingana na mwongozo na sheria za maji Na. 12. Hadi sasa Jumuiya ya watumiaji maji 13 zimeundwa Mtimbira ,Kiswago,Sofi majiji ,Sofi Mission,Misegese,Igawa,Kiwale,Mchangani,Biro,Mbalinyi,Ngoheranga ,Mabanda na Kilosa Mpepo.

6.0 HITIMISHO

Pamoja na changamoto za uhaba mkubwa wa watumishi,vitendea kazi idara inaendelea kusimamia miradi kwaajiliya kuhakikisha hudumaya maji inaboreshwa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia yote

Habari za hivi punde

  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA MALINYI ATOA WITO KWA WAKAZI WA MALINYI KUJITOKEZA KUJIANDIKISHA NA KUHAKIKI TAARIFA ZAO

    May 16, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MALINYI AWATAKA WATENDAJI KATA NA VIJIJI KUHAKIKISHA WANAFUNZI WOTE WANAPATA CHAKULA CHA MCHANA SHULENI

    May 15, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MALINYI AWATAKA WATENDAJI KATA NA VIJIJI KUHAKIKISHA WANAFUNZI WOTE WANAPATA CHAKULA CHA MCHANA SHUKENI

    May 15, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA MALINYI KHAMIS KATIMBA AFUNGUA MAFUNZO KWA WATENDAJI WA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA JIMBO LA MALINYI AWMU YA PILI

    May 14, 2025
  • Angalia yote

Video

DAS MALINYI AKIKABIDHI PIKIPIKI KWA WARATIBU ELIMU KATA
Video zaidi

Tovuti za haraka

  • Matangazo
  • Habari za Hivi punde

Tovuti Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Tovuti ya Ajira
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2022
  • Matokeo ya Kidato cha Nne
  • SALARY SLIP PORTAL
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2018

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi

    Postal Address: 18 Malinyi, Morogoro

    Telephone: 0643111999

    Mobile:

    Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.