Halmashauri ya wilaya ya malinyi mkoani morogoro inatarajia kuanza utekelezaji wa zoezi la
uwekaji wa hereni za kieletroniki kwa mifugo ya ng'ombe,punda,kondoo na mbuzi kwa lengo la
kutambua idadi ya mifugo iliyopo pamoja na kudhibiti ongezeko la mifugo hiyo.
Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani kaimu afisa mifugo wa halmashauri ya wilaya ya
malinyi bwana Goodluck Mosha amesema zoezi la uwekaji wa hereni za kieletroniki ni mbadala
wa zoezi kama hilo ambapo awali mifugo ilikuwa ikiwekwa alama kwa kupigwa chapa ambazo
baadae zilifutika na hivyo kufanya serikali kukosa taarifa sahihi za idadi kamili ya mifugo iliyopo
nchini.
Bwana Mosha ameongeza kuwa zoezi hilo limekuja wakati ambapo halmashauri tayari
ilishapitisha bajeti na kutoa fursa kwa mawakala kuendesha zoezi hilo ambapo kila mfugaji
atalazimika kutoa shilingi 1750 kwa kila ng'ombe na punda na shilingi 1000 kwa kila kondoo na
mbuzi huku kiasi kidogo kinachotokana na mapato ya zoezi hilo yakibaki katika halmashauri.
Aidha bwana mosha amesema kwa kuwa mifugo inatayotakiwa kuvishwa hereni hizo ni ile
iliyofikisha umri wa miezi mitatu na kuendelea hivyo hilo ni zoezi endelevu kwa kila mwaka hivyo
basi halmashauri inaendelea kujipanga ambapo baadae itaanza kusimamia zoezi hilo na
kunufaika zaidi na mapato yatokanayo na zoezi hilo.
Zoezi la uwekaji wa hereni kwa mifugo limekuja kufuatia agizo la serikali kupitia wizara ya
mifugo na uvuvi la kutaka halmashauri zote nchini kufanya hivyo ili kuiwezesha serikali kupata
taarifa kamili juu ya idadi ya mifugo yote iliyopo nchini iliiweze kuisimamia ikiwa ni pamoja na
kutafuta masoko ya kimataifa kwa lengo la kuwafanya wafugaji kuwa na soko la uhakika.
Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi
Postal Address: 18 Malinyi, Morogoro
Telephone: 0643111999
Mobile:
Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz
Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.