• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Malinyi District Council
Malinyi District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
      • Mipango
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Machine Investment
    • Skimu ya Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili Madiwani
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Kata
      • Biro
      • Igawa
      • Itete
      • Kilosa Mpepo
      • Mtimbira
      • Malinyi
      • Njiwa
      • Ngoheranga
      • Sofi
      • Usangule
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Matamko ya mbalimbali
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video

MALINYI YAONGOZA MATEMBEZI YA HISANI KUHAMASISHA UANDIKISHAJI WAPIGA KURA

Posted on: October 14th, 2024

 

Wilaya ya Malinyi Oktoba 13, 2024 Imeongoza matembezi ya hisani ya Zaidi ya kilometa 3 kuhamasisha Wananchi wa Wilaya ya Malinyi kujiandikisha katika orodha ya Wapiga kura zoezi ambalo lilianza rasmi Oktoba 11 na litarajiwa kukamilika Oktoba 20, 2024


Matembezi hayo ya hisani yamefanyika katika Tarafa 3 za Wilaya ya Malinyi ambapo Tarafa ya Malinyi Mhe. Sebastian Waryuba ameongoza Wananchi katika matembezi hayo, Tarafa ya Mtimbira Katibu Tawala wa Wilaya Bi Saida Mhanga amewaongoza Wananchi, na Tarafa ya Ngoheranga Msimamizi wa Uchaguzi Malinyi Ndugu Khamis Jaaphar Katimba ameongoza Wananchi katika matembezi hayo.


Matembezi ya hisani Malinyi pia yamelenga kuadhimisha kumbukizi ya miaka 25 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ikiwa ni pamoja na kuhitimisha mbio za Mwenge wa Uhuru tukio ambalo limefanyika Oktoba 13, 2024 Jijini Mwanza.


Akizungumza na Washiriki wa matembezi ya hisani katika Tarafa ya Malinyi DC Waryuba amesema kuwa Ili kushiriki Uchaguzi wa Serikali za mitaa sio lazima uwe na kadi au kitambulisho cha mpiga kura, ukiwa na miaka 18 na kuendelea unaruhusiwa kwenda kujiandikisha katika kituo kilicho karibu yako.


DC Waryuba pia amesema kuwa Uchaguzi wa Serikali za mitaa ni Uchaguzi wa Serikali za wenyeji, watu wanaohusika katika eneo hilo, hiyo ni vyema kuhakikisha kuwa wenyeji wote wa Malinyi wanashiriki kikamilifu katika kujiandikisha na kupiga kura .


Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Malinyi Bi Saida Mhanga amewaomba wakazi wa Tarafa ya Mtimbira na Wilaya nzima ya Malinyi kujijitokeze kujiandikisha ili wawe na sifa ya kuchagua Viongozi wanaowataka kwa maendeleo ya Malinyi.

Aidha Bi saida Mhanga ametoa rai kwa Wananchi wote wa Malinyi wenye umri wa miaka 21 na kuendelea kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika maeneo yao.


Kwa upande wake Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Malinyi Ndugu Khamis Jaaphar Katimba amesema kuwa zoezi la matembezi ya hisani limehusisha Vijana kwa kiasi kikubwa ili vijana hao wapeleke ujumbe wa kujiandikisha na kupiga kura kwa Vijana wenzao pamoja na wazazi wao.


Akizungumzia suala la usalama tangu zoezi la uandikishaji lilipozinduliwa rasmi Msimamizi huyo wa uchaguzi ameeleza kuwa zoezi hilo linaendelea vizuri hakuna dosari kubwa zilizojitokeza na kuongeza kuwa uhamasishaji unaendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali ya Malinyi ili kujenga uelewa Zaidi kwa Wananchi.


 Hata hivyo, Ndugu Katimba mara baada ya kukamilisha zoezi la matembezi ya hisani katika Tarafa ya Mtimbira amefanya mkutano na vyama vyote vinavyoshiriki Uchaguzi wa Serikali za mitaa Wilayani Malinyi ili kufanya tathimini pamoja ya zoezi la uandikishaji tangu lilipozinduliwa rasmi Oktoba 11, 2024 na kuongeza kuwa Malinyi inatarajia kuandikisha wapiga kura Zaidi ya 100,00.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia yote

Habari za hivi punde

  • SERIKALI YATENGA SH. BILIONI 18 KWAAJILI YA UJENZI WA MADARAJA MAWILI WILAYANI MALINYI

    April 24, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MALINYI YAPONGEZWA KWA UKUSANYAJI WA MAPATO

    April 24, 2025
  • KESI ZOTE ZA MIGOGORO YA ARDHI SASA KUSAJILIWA NA KUSIKILIZWA MALINYI

    March 24, 2025
  • "ITISHENI MIKUTANO YA VIJIJI"

    March 20, 2025
  • Angalia yote

Video

DAS MALINYI AKIKABIDHI PIKIPIKI KWA WARATIBU ELIMU KATA
Video zaidi

Tovuti za haraka

  • Matangazo
  • Habari za Hivi punde

Tovuti Mashuhuri

  • Tamisemi
  • Tovuti ya Ajira
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2022
  • Matokeo ya Kidato cha Nne
  • SALARY SLIP PORTAL
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2018

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi

    Postal Address: 18 Malinyi, Morogoro

    Telephone: 0643111999

    Mobile:

    Barua pepe za watumishi: ded@malinyidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.